Loading...
ADVERTISE WITH US ON THIS BLOG.CALL +255 714 789 592/ +255 682 997 767/ +255 752 944 022

Wakala Wa Huduma Za Misitu Tanzania (TFS) Yakabidhi Madawati 50 Kwa Halmashauri ya Mji Wa Masasi.

TANGAZO
 MENEJA msaidizi wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) Kanda ya Kusini Boaz Sanga (Kulia) akimkabidhi kaimu mkurugenzi wa Halmashauri ya mji wa Masasi Joram Msyangi msaada wa madawati 50 yaliyotolewa kwa Halmashauri hiyo hii leo.

Na Clarence Chilumba,Masasi.
WAKALA  wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) Kanda ya Kusini imekabidhi msaada wa madawati 50 kwa Halmashauri ya mji wa Masasi mkoani Mtwara,lengo likiwa ni kuunga mkono jitihada za serikali ya awamu ya tano katika kutatua kero ya madawati kwa shule za msingi na sekondari nchini.

Msaada huo wa Madawati 50 wenye thamani ya shilingi milioni 5.2 umekabidhiwa hii leo kwa mratibu wa mfuko wa maendeleo ya jamii nchini (TASAF) Joram Msyangi aliyemwakilisha mkurugenzi wa Halmashauri ya mji wa Masasi Fortunatus Kagoro.

Akizungumza wakati wa makabidhiano ya msaada huo meneja msaidizi usimamizi wa Rasilimali za misitu kanda ya Kusini Boaz Sanga alisema wamefikia hatua ya kutoa msaada huo ili kumuunga mkono Rais Dk.John Pombe Magufuli.

Alisema wameamua kutengeneza madawati hayo kwa kutumia mbao walizozikamata kutoka kwa wafanyabiashara waliowakamata wakisafirisha mbao hizo kinyume na sheria za misitu zilizowekwa na serikali.

“Huu ni mwanzo tu tumejipanga kuendelea kutengeneza madawati mengine kadri tutakavyoweza…lengo ni kuiunga mkono serikali katika kuhakikisha kila mtoto wa kitanzania anakaa kwenye dawati”alisema Sanga.

Kwa upande wake kaimu mkurugenzi wa Halmashauri ya mji wa Masasi Joram Msyangi alisema msaada huo umekuja kwa wakati muafaka kwani kwa mujibu wa agizo la Rais inazitaka Halmashauri zote nchini kukamilisha zoezi la madawati ifikapo june 30, 2016.

Alisema Halmashauri ya mji imekuwa ikifanya jitihada mbalimbali ikiwemo kukarabati na kutengeneza madawati hayo sambamba na kutumia taasisi mbalimbali za serikali na zisizo za kiserikali ili kutekeleza agizo hilo kwa wakati uliopangwa.


 BAADHI ya wanafunzi wa shule za sekondari Halmashauri ya mji wa Masasi wakiwa wamekaa kwenye madawati baada ya kukabidhiwa kutoka kwa TFS.




MADAWATI yaliyokabidhiwa hii leo na wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) kwa Halmashauri ya Mji wa Masasi.
TANGAZO
Facebook Blogger Plugin by WAYEGE CO.LTD
Newer Posts Older Posts
© Copyright Mtazamo Mpya | Designed By FAHARI YA TANZANIA
Back To Top