Loading...
ADVERTISE WITH US ON THIS BLOG.CALL +255 714 789 592/ +255 682 997 767/ +255 752 944 022

WAUMINI WA JUMUIYA YA WAISLAMU WA AHMADIYA NCHINI WATAKIWA KUHUBIRI AMANI NA UPENDO

TANGAZO
Sheikh Alli Dino Tahir wa Kanda ya Kusini Jumuiya ya Ahmadiya.

Na Clarence Chilumba,Masasi.
Amir na mbashiri mkuu wa jumuiya ya waislamu wa Ahmadiya nchini Tahir Chandry amewataka waumini wa jumuiya hiyo kumtumikia mungu kikamilifu kwa kufuata misingi na kanuni zilizowekwa katika Quran tukufu kwa lengo la kuleta amani na mshikamano miongoni mwa waislamu wa jumuiya hiyo duniani.
Akizungumza jana mjini Masasi wakati wa mkutano mkuu wa mwaka wa jumuiya hiyo kwenye viwanja vya msikiti wa Ahmadiya mjini humo alisema lengo la kuanzishwa kwa jumuiya hiyo ni kuwaunganisha waumini wote wenye kufuata amri zilizowekwa na mwenyezi mungu.
Alisema mafundisho kutoka katika vitabu vitakatifu mungu amehimiza amani,upendo,na mshikamano kwa wale wote wanaomwanini kwa nia thabiti na kwamba hali ilivyo kwa sasa ni tofauti kwani kumezuka makundi mbalimbali ya dini ya kiislamu yapatayo 72 ulimwenguni kote huku kila moja likijinadi kuwa ndilo linalofuata maagizo yaliyopo kwenye kitabu kitakatifu cha Quran tukufu.
Alisema uelewa mdogo kuhusu dini ya kiislamu kwa baadhi ya waumini wa dini hiyo ndiko kulikopelekea kuwepo kwa tofauti kubwa kote duniani mazingira ambayo hupelekea waislamu kuuana wenyewe kwa wenyewe ikiwemo mauaji yanayotekelezwa na makundi mbalimbali kama vile Boko Haram,Al Shabab na mengineyo.
Kwa mujibu wa Amir na mbashiri mkuu wa jumuiya ya Ahmadiya nchini Tahir alisema wakati umefika kwa waislamu kufuata kamba iliyo ya kweli ya mwenyezi mungu na kwamba wao kama jumuiya moja ya kazi kubwa wanayoifanya kwa sasa ni kuhubiri amani kote ulimwenguni ili waislamu wamrudie mungu wao sambamba na kuacha mapigano ya kila siku yanayosababisha maelfu ya waislamu kupoteza maisha.
“Kila siku kupitia vyombo vya habari vya kimataifa tumekuwa tukishuhudia mauaji ya waislamu kule Yemen,Pakistan…lakini ukiangalia kiundani zaidi wanaotekeleza mauaji yale ni waislamu ambao huua waislamu wenzao na wakati mwingine hata wasio waislamu huuawa kwa nini tuendelee kuuana huku kamba sahihi ya uzima ipo inayofuata ukhalifa”.alisema Amir Chandry.
Akizungumzia namna jumuiya yake inavyounga mkono jitihada za serikali ya Tanzania katika kuboresha miundo mbinu mbalimbali ikiwemo elimu,afya na maji Amir Chandry alisema wamefanikiwa kuchimba na kujenga visima vya maji katika baadhi ya maeneo nchini ikiwemo mikoa ya Mtwara,Morogoro,Dodoma,Singida pamoja na Arusha.
Alisema mbali na kujenga visima vya maji pia jumuiya ya waislamu wa Ahmadiya nchini imekuwa ikitoa misaada katika shule mbalimbali za sekondari kama vile kompyuta,madawati pamoja na vitabu kwa wanafunzi wa shule hizo na kwamba kote wanakopita hutoa mahubiri kuhusu amani na namna ya kuifuata kamba bora ya imani kitu ambacho amekiri kuwa ni tofauti na baadhi ya jumuiya zingine.
Kuhusu uchaguzi mkuu wa Tanzania Oktoba mwaka huu Amir alisema wao kama jumuiya ya Ahmadiya wako tayari kufuata kanuni na taratibu za nchi kwa Rais yeyote ambaye atachaguliwa na watanzania na kwamba wao kama jumuiya ya kidini nchini hawawezi kuwahubiria waumini wao ni kiongozi yupi na wa chama gani anafaa kuwa Rais wa awamu ya tano wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania.
Jumuiya ya waislamu wa Ahmadiya ilianzishwa machi 23,1889 huko nchini India na kwamba hadi sasa jumuiya hiyo imefikisha umri wa miaka 126 ikiwa na wafuasi milioni 200 kwenye nchi takribani 206 kote ulimwenguni.
Mwisho.

Waumini wa Jumuiya ya Ahmadiya Mjini Masasi wakifuatilia kwa ukaribu mada mbalimbali zilizokuwa zikiwakilishwa na walimu wa jumuiya hiyo kutoka maeneo mbalimbali ya mikoa ya Kanda ya Kusini.
Amir na Mbashiri Mkuu wa Jumuiya ya Waislam ya Ahmadiya Tahir Mohammood Chandry (Kulia) akiongea na mwandishi wa Blog ya Mtazamo mpya jana baada ya kumaliza mahubiri yake. kushoto ni Sheikh Mohamed Hafudhar Batti-sheikh wa Jumuiya ya Ahmadiya Mkoa wa Tanga.

Kutoka kushoto ni Amir na mbashiri mkuu wa jumuiya ya Ahmadiya Tahir Mohammood Chandry,Sheikh Mohamed Hafudhar Batti wa Mkoa wa Tanga pamoja na Sheikh Kalindima wa Newala wakiwa kwenye viwanja vya msikiti wa Jumuiya ya Ahmadiya mjini Masasi .
Baadhi ya viongozi na walimu mbalimbali wa Jumuiya ya Ahmadiya wakifuatilia mada mbalimbali kutoka kwa viongozi wa juu wa jumuiya hiyo.
TANGAZO
Facebook Blogger Plugin by WAYEGE CO.LTD
Newer Posts Older Posts
© Copyright Mtazamo Mpya | Designed By FAHARI YA TANZANIA
Back To Top